• Login
    • Login
    Advanced Search
    View Item 
    •   Maseno IR Home
    • Journal Articles
    • School of Arts and Social Sciences
    • Department of Kiswahili & Other African Languages
    • View Item
    •   Maseno IR Home
    • Journal Articles
    • School of Arts and Social Sciences
    • Department of Kiswahili & Other African Languages
    • View Item
    JavaScript is disabled for your browser. Some features of this site may not work without it.

    Mitindo ya Lugha Inayowabainisha Wahusika Wazimu katika Riwaya za Habwe

    Thumbnail
    View/Open
    document (2).pdf (299.2Kb)
    Publication Date
    2023-07-31
    Author
    Odhong’, Joseph Ondiek
    Amukowa, Debora Nanyama
    Asiko, Beverlyne Ambuyo
    Metadata
    Show full item record
    Abstract/Overview
    Takwimu za Shirika la Afya Ulimwenguni zinaonyesha ongezeko la idadi ya wazimu katika jamii duniani kote (Kovacevic, 2021). Waandishi wa fasihi wamewaumba wahusika wazimu wakiakisi mazingira wanamoishi. Tangu jadi wahakiki wamejitahidi kueleza vipi wahusika wazimu wametumika katika fasihi. Tahakiki za tamthilia za Shakespeare na za Kiingereza za karne ya ishirini zimeeleza namna na sababu za uumbaji wao. Katika riwaya za Kiswahili hakuna tahakiki zinazoshughulikia wahusika wazimu wala mitindo ya lugha inayowabainisha. Makala hii ilidhamiria kuchanganua mitindo ya lugha inayowabainisha wahusika wazimu katika kazi teule za Habwe. Uteuzi huu ulitokana na Habwe kusifiwa kuwa mwandishi wa fasihi ya kiongofu aliyetumia motifu ya wazimu katika riwaya zake (Gromov, 2018). Riwaya tano za Habwe: Paradiso (2005), Cheche za Moto (2008), Fumbo La Maisha (2009), Safari ya Lamu (2011) na Kovu Moyoni (2014) ziliteuliwa kupitia usampulishaji dhamirifu kwa kuwa zilikuwa na wahusika wazimu. Nadharia ya umitindo iliyoasisiwa na Bally (1909) ) na kuendelezwa na Thornborrow na Wareing (1998) iliteuliwa kwa ajili ya kazi hii. Muundo wa kiuchanganuzi umetumiwa. Data zilikusanywa kutumia kifaa cha kudondoa data kilichokuwa na vidokezo vya mitindo ya lugha inayotambulisha wahusika wazimu. Matini ya riwaya teule imesomwa kwa makini na vipengele mbalimbali, kurekodiwa. Kisha data imechanganuliwa, kufasiriwa na kuratibiwa kulingana na madhumuni ya utafiti. Matokeo yamewasillishwa kwa njia ya maelezo. Makala hii imedhihirisha jinsi mitindo ya lugha ilivyotumiwa kuwatambulisha wahusika wazimu.
    Permalink
    https://repository.maseno.ac.ke/handle/123456789/5841
    Collections
    • Department of Kiswahili & Other African Languages [38]

    Maseno University. All rights reserved | Copyright © 2022 
    Contact Us | Send Feedback

     

     

    Browse

    All of Maseno IRCommunities & CollectionsBy Issue DateAuthorsTitlesSubjectsThis CollectionBy Issue DateAuthorsTitlesSubjects

    My Account

    LoginRegister

    Statistics

    View Usage Statistics

    Maseno University. All rights reserved | Copyright © 2022 
    Contact Us | Send Feedback