• Login
    • Login
    Advanced Search
    View Item 
    •   Maseno IR Home
    • Journal Articles
    • School of Arts and Social Sciences
    • Department of Kiswahili & Other African Languages
    • View Item
    •   Maseno IR Home
    • Journal Articles
    • School of Arts and Social Sciences
    • Department of Kiswahili & Other African Languages
    • View Item
    JavaScript is disabled for your browser. Some features of this site may not work without it.

    Nafasi ya Ikolojia ya Lugha katika Mtagusano wa Kiswahili na Kibukusu katika Mawanda ya Dini katika Kaunti ya Bungoma

    Thumbnail
    View/Open
    document (6).pdf (354.8Kb)
    Publication Date
    2023-03-27
    Author
    Barasa Martin Mulwale, Ngesa Florence Indede, Asiko Beverlyne Ambuyo
    Metadata
    Show full item record
    Abstract/Overview
    Nyanja mbalimbali katika jamii hutegemea matumizi ya lugha. Hali hii huzua changamoto ya namna ya kutumia raslimali za lugha zinazopatikana katika jamiilugha fulani. Juhudi ya kufahamu na kutagusana na ulimwengu huhitaji matumizi ya kiisimu ya kipekee. Katika muktadha wa kidini kuna changamoto ya asili ya maneno, mamlaka, utambulisho na ushirikiano wa wahusika. Aidha, miktadha mbalimbali ya kidini hutumia lugha kutimiza mahitaji yake maalum. Lugha hutenda matendo, huomba maombi ya kukemea, husimulia hali za kijamii na hata huonekana kudhibiti matendo ya Maulana. Ni kwa misingi hii ndipo kazi hii inajukumika kutalii jinsi lugha ya Kiswahili na Kibukusu zinavyotagusana katika mawanda haya ya dini, hasa Dini ya Musambwa (DYM) ambayo inaaminika kuwa ya kiasili katika jamii hii ya Wabukusu katika Kaunti ya Bungoma. Kazi hii inazingatia misingi ya Spolsky (2004, 2006, 2009) ambaye anajadili kuwa sera ya lugha halisi ya jamii hupatikana kwenye matumizi yake. Anazingatia Mwelekeo wa ikolojia ya lugha uliozinduliwa na Haugen (1972) unaochunguza mwingiliano baina ya lugha na mazingira. Muundo wa kiuchanganuzi ulitumiwa. Kupitia uchunzaji wa kutoshiriki moja kwa moja mtafiti alihudhuria ibada na kunasa mazungumzo yao kwenye kanda ya kunasia sauti. Mazungumzo hayo yalinakiliwa na orodha ya uchunzaji ilitumiwa kubainisha na kueleza namna lugha ya Kibukusu na Kiswahili zilivyotumiwa katika shughuli za kanisa hilo. Hali ya kuchanganya na kubadili msimbo, utohozi na hata matumizi ya Kiswahili kwa Kibukusu haikuweza kuepukika. Utafiti huu unadhihirisha kuwa raslimali za lugha zilizopo katika ikolojia fulani huchagizana katika kukamilisha majukumu ya mawasiliano katika muktadha husika.
    Permalink
    https://repository.maseno.ac.ke/handle/123456789/5673
    Collections
    • Department of Kiswahili & Other African Languages [38]

    Maseno University. All rights reserved | Copyright © 2022 
    Contact Us | Send Feedback

     

     

    Browse

    All of Maseno IRCommunities & CollectionsBy Issue DateAuthorsTitlesSubjectsThis CollectionBy Issue DateAuthorsTitlesSubjects

    My Account

    LoginRegister

    Statistics

    View Usage Statistics

    Maseno University. All rights reserved | Copyright © 2022 
    Contact Us | Send Feedback