• Login
    • Login
    Advanced Search
    View Item 
    •   Maseno IR Home
    • Journal Articles
    • School of Arts and Social Sciences
    • Department of Kiswahili & Other African Languages
    • View Item
    •   Maseno IR Home
    • Journal Articles
    • School of Arts and Social Sciences
    • Department of Kiswahili & Other African Languages
    • View Item
    JavaScript is disabled for your browser. Some features of this site may not work without it.

    Jinsi Mtindo Katika Ushairi Unavyofundishwa Katika Shule za Upili: Mfano wa Kaunti Ndogo ya Teso Kaskazini, Kaunti ya Busia, Kenya

    Thumbnail
    View/Open
    document (7).pdf (177.1Kb)
    Publication Date
    2019
    Author
    9. Mukoya, H., Wasike, M., Amukowa, D., & Masinde, E
    Metadata
    Show full item record
    Abstract/Overview
    Makala hii inahusu jinsi ambavyo mtindo katika ushairi unavyofundishwa katika shule za upili nchini Kenya. Wasomi mbalimbali wametafiti kuhusiana na jinsi ambavyo vipengee tofautitofauti vya ushairi vinavyobainika. Aidha, wasomi hao wametafiti kuhusiana nanamna ya kufundisha ushairi. Japo tafiti nyingi zimefanywa kuhusiana na ushairi, pana haja kubwa ya kufanya utafiti kuhusiana na jinsi ya kufundisha mtindo katika ushairi. Hiki ndicho kichocheo cha makala hii. Utafiti huu uliongozwa na nadharia ya utanzu iliyoasisiwa na Boasna kuendelezwa naye Bakhtin. Nadharia hii ina mihimili kadhaa lakini mhimiliunaoshikilia kuwa tanzu huibua muundo wa kazi fulani ya fasihi na kufanya kazihiyo ieleweke kwa urahisi sana, ndio uliotumika katika utafiti huu.Utafiti huu ulitumia sampuli ya utabakishaji kuteua shule zilizoshiriki utafiti huu. Sampuli ya kimakusudi ilitumiwa kuteua walimu kwa sababu hao ndio walio na mamlaka ya kufundisha. Kaunti Ndogo ya Teso Kaskazini ina shule thelathini (30), hivyo basi utafiti ulizingatia asilimia thelathini (30%) kwa kuteua shule tisa (9). Utafiti huu ulitumia mbinu ya usaili nambinu ya uchunzaji kukusanya data zilizohitajika.Matokeo ya utafiti yalionyesha kuwa walimu walitumia maigizo, maswalina majibu, kazimradi, majadiliano, vikundi vya majadiliano, kanda au santuri, kukariri, kinuruweo na maelezo kama mbinu za ufundishaji kufundishia mtindo katika ushairi.Utafiti huu unapendekeza kuwawalimu wa Kiswahili watilie maanani mbinu mahususi wanapofundisha ushairi ili wanafunzi wachangamkie somo la ushairi. Vilevile, unapendekeza kuwa taasisi zinazokuza mitaala ziweze kuzingatia pakubwa sana mbinu mahususi ambazo zitatumiwa na walimu kwa ajili ya kuboresha zaidi ufundishaji wa ushairi. Aidha, unapendekeza kuwa tafiti nyingine zifanywe kuhusiana na jinsi ya kufundisha vipengee vingine vya ushairi kando na mtindo.
    Permalink
    https://repository.maseno.ac.ke/handle/123456789/4889
    Collections
    • Department of Kiswahili & Other African Languages [38]

    Maseno University. All rights reserved | Copyright © 2022 
    Contact Us | Send Feedback

     

     

    Browse

    All of Maseno IRCommunities & CollectionsBy Issue DateAuthorsTitlesSubjectsThis CollectionBy Issue DateAuthorsTitlesSubjects

    My Account

    LoginRegister

    Statistics

    View Usage Statistics

    Maseno University. All rights reserved | Copyright © 2022 
    Contact Us | Send Feedback