Show simple item record

dc.contributor.authorOkal, Benard Odoyo
dc.date.accessioned2024-07-31T13:47:10Z
dc.date.available2024-07-31T13:47:10Z
dc.date.issued2024-04-11
dc.identifier.urihttps://repository.maseno.ac.ke/handle/123456789/6126
dc.description.abstractKamusi kadhaa wahidiya (za lugha moja) za Kiswahili kama vile Kamusi ya Kiswahili Sanifu toleo la kwanza, pili na tatu, zimewahi kutungwa kutokana na juhudi za Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili (TUKI) inayojulikana sasa kama Taasisi ya Taaluma za Kiswahili (TATAKI) ili kusaidia mafunzo ya Kiswahili na taaluma ya leksikografia katika taasisi kadhaa za elimu. Kamusi nyingi wahidiya za Kiswahili zimetungwa kwa kutumia mitindo anuwai ya utoaji maelezo ya taarifa muhimu za vidahizo husika licha ya kwamba kuna lugha kienzo maalum ya kuzingatiwa katika kuwasilisha taarifa hizo za vidahizo. Hivyo basi, makala haya yanahakiki kiulinganifu wa taarifa muhimu kuhusu vidahizo katika Kamusi ya Kiswahili Sanifu toleo la tatu (TUKI, 2013) na Kamusi ya Karne ya 21 (Mdee, Njogu na Shafi, 2011). Uhakikiki linganishi katika makala haya umehusisha masuala anuwai hasa maelezo ya idadi ya vidahizo, mpangilio wa vidahizo, taarifa za kisarufi (tahajia na matamshi, kategoria ya kidahizo, ngeli, uelekezi wa vitenzi, mofolojia hasa minyambuliko ya vidahizo, maana na matumizi ya vidahizo katika miktadha anuwai) pamoja na vipengee vingine vya lugha kienzo ya msimbo kwa mujibu wa taaluma ya leksikografia.en_US
dc.publisherUniversity of Dar es saalamen_US
dc.titleUhakiki linganishi wa taarifa muhimu kuhusu vidahizo katika kamusi ya karne ya 21 na kamusi ya Kiswahili sanifuen_US
dc.typeArticleen_US


Files in this item

Thumbnail

This item appears in the following Collection(s)

Show simple item record